Back to Religious Books

Wacha Mungu wa Zama za Digitali

2 reviews
100% of buyers enjoyed this product!

Sh 1,500.00

➡ Mtunzi: Baraka Oscar Mung’ong’o
➡ Aina: Kitabu cha Kidigitali
➡ Mwaka: 2015
➡ Kurasa: 222
➡ ISBN 978 9987 9970 0 8
➡ Mchapishaji: Trisoftnet Incorporation Limited
➡ Mhariri Mkuu: Ezekiel Milembe
➡ Unaweza Kukipakua ndani ya dakika 5 – 30

1000000 in stock

SKU:
VT01
Buyer protection
Safe shopping
Easy returns and refunds
Free shipping worldwide

Wacha Mungu wa Zama za Digitali

Wacha Mungu wa zama za digitali ni kitabu kinachoelezea mapinduzi makubwa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) yanagusa maisha ya wacha Mungu kwa namna tofauti tofauti. Jambo hili linapelekea mabadiliko makubwa katika mawasiliano yanayolitishia Kanisa la Mungu na misingi yake. Namna watu wanavyowasiliana katika zama hizi za digitali kumeongeza kasi ya kubadilishana taarifa. Kasi hii ndiyo aliyoiona Daniel katika unabii wake wa zama za mwisho wa misingi ya dunia.

Shetani anatumia fursa hii ya haya maarifa makubwa kueneza uovu wake kwa kasi. Ili kutambua namna ya kujiweka salama katika zama hizi ni vyema kuzing’amua njia salama zinazopaswa kutumika wakati wa kufanya mawasiliano. Msingi wa matatizo yote ulimwenguni kwa asilimia 85% husababishwa na namna ya kuwasiliana.

Shetani alivyokuwa akiwasiliana na Eva katika bustani ya Edeni, alitumia mawasiliano vibaya na kufanikiwa kumhadaa Eva naye akamhadaa mume wake Adamu. Kwa kasi iliyo kubwa zaidi, Shetani aliye baba wa uongo ameendelea kutumia mapinduzi ya TEHAMA kwa namna ya upotofu ili kuangamiza roho yumkini hata za wateule wa Mungu.

Kitabu hiki ni maalum kwa ajili yako ili uweze kutambua changamoto ambazo unaweza kuzipata kama baba, mama au mtoto kutokana na matumizi ya Teknolojia Ya Habari Na Mawasiliano. Watu wengi wameumizwa na Mitandao kiasi wamejikuta wakibadili tabia au maadili yao.

Ufahamu mdogo wa mambo mengi unachangia sana mtu kufanya uchaguzi usio sahihi. Matumizi ya vitumizi vya mawasiliano vya kidigitali kama rununu, sikanu, tabiti, ngamizi na runinga yamekuwa yakiathiri sana mitindo ya maisha. Licha ya ukweli kwamba utamaduni hutoa miongozo mingi ya kimaisha bado kuna mambo ambayo hayapaswi kufanywa na wacha Mungu kwa sababu ya mapinduzi ya TEHAMA.

Maandiko Matakatifu yana nafasi kubwa sana ya kuonya na kuwaongoza wacha Mungu. Maana kila Neno la Mungu lafaa kwa mafundisho. Unapopata muda wa kuyachunguza Maandikio, tafakari pia mwenendo wako wa maisha. “Je, ni kwa kiasi gani simu yako imeyabadili maisha yako?” Maisha yameathirika kwa kiwango kikubwa katika nyanja ya mtu mmoja mmoja mpaka familia. Ni makosa gani umekuwa ukiyafanya kila siku kwa sababu ya kutumia simu? Ni wajibu wetu kuyatambua yale yanayotokea katika maisha yetu kama yanapaswa kufanywa au kuachwa. Ugunduzi wa maarifa makubwa ya mawasiliano unawagusa watu wote. Maarifa haya yamekuwa na athari chanya na hasi kwa wacha Mungu na wamejikuta wakiacha misingi ya imani zao.

Maudhui ya kitabu hiki ni kuwaonesha wacha Mungu njia salama za kuzingatia katika zama hizi za digitali ili maarifa haya makubwa ya mawasiliano yasipofushe ufahamu wao juu ya Mungu. Kupoteza kibali mbele za Mungu kwa sababu ya simu ni jambo la hatari na halipaswi kuachwa liwaangamize wacha Mungu.

Kuna baadhi ya maneno yametumika katika kitabu hiki yanaweza kuwa ni mageni kwako. Ili kuwa na uelewa mzuri wa kile kinachoelezwa ni vizuri ukasoma sehemu ya mwisho kabisa ya ‘Ufafanuzi wa Maneno’ kabla ya kuanza kusoma kitabu hiki. Sehemu hii itakupa tafsiri rahisi ya kila msamiati mpya uliotumika. Kwa kufanya hivyo utakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuelewa maudhui ya kitabu hiki. Lengo kubwa ni kuhakikisha kuwa wacha Mungu wanabakia salama licha ya matumizi yasiyo na staha yanayofanywa na watumiaji wengi wa vitumi vya mawasiliano vya kidigitali na mapinduzi yake.

Maisha ni kuchagua. Mungu alitupa uhuru wa kuchagua tangu mwanzo. Mbele yetu kuna uzima na mauti, chagua uzima ili umwone Mungu. Simu yako isije ikapelekea mauti yako na ya wale uwapendao. Jifunze njia sahihi za kukabiliana na mapinduzi ya TEHAMA katika zama za digitali kabla hujachelewa.
Simu, rununu, sikanu, tabiti, ngamizi, Mtandao na runinga ni vifaa tu vya mawasiliano. Isije ikatokea mtu anaikosa Mbingu mpya na Nchi ile mpya kwa sababu ya vifaa hivi. Hakikisha matumizi ya vifaa vya kidigitali hayakutengi na Mungu siku zote za uhai wako. Wala usikubali kuikosa Mbingu kwa sababu ya mawasiliano mabaya. Laiti ungelijua kile ambacho Yesu Kristo amekuandalia basi ungefanya bidii ili upate kumwona uso wake.

Ushindi katika maisha yetu tunaupata kupitia yeye maana alishaishinda dhambi msalabani. Licha ya uwepo wa zama za kutisha zenye ubinafsi mkubwa kutokana na kukua kwa maarifa bado watu wa Mungu wanapaswa kujipambanua katika mwonekano tofauti na wa ulimwengu hasa wanapozingatia kuwa huu ulimwengu ni wa kupita na makazi yao yapo Mbinguni.

Mungu ameahidi kuja kuishi na wanadamu katika mbingu mpya na nchi mpya. Mpango wake ni wa hakika. Hata hivyo ipo kazi ya kufanya kwa kuhakikisha ulimwengu na maarifa yake yote haukuangamizi milele. Mungu akubariki unaposoma kitabu hiki chenye wingi wa maarifa ya nyakati hizi.

YALIYOMO

➡ Shukrani…. 3
➡ Dibaji… 4
➡ Utangulizi … 5
➡ SURA YA KWANZA:  Hofu Yangu …. 6
➡ SURA YA PILI: Mianzo Ya Mawasiliano… 15
➡ SURA YA TATU: Umuhimu Wa Mawasiliano… 37
➡ SURA YA NNE Dhana Potofu Kuhusu Mawasiliano… 48
➡ SURA YA TANO: Kero Za Rununu … 58
➡ SURA YA SITA: Changamoto Za Digitali Kwa Wacha Mungu… 69
➡ SURA YA SABA: Matumizi Salama Ya Vitumi Vya Mawasiliano … 145
➡ SURA YA NANE: Maadili Na Miiko Ya Teknolojia Ya Habari Na Mawasiliano… 189
➡ SURA YA TISA: Njozi Kwa Kanisa La Masalia… 208
➡ Ufahamu wa Maneno … 221

Onyo

Haki Zote Zimehifadhiwa. Huruhusiwi kutoa nakala ya kitabu hiki au sehemu ya kitabu hiki kwa sababu yoyote ile bila ruhusa ya mmliki wa kitabu kwa maandishi. Juhudi zimetumika kuandaa kitabu hiki kwa usahihi na umakini mkubwa sana kwa lengo la kutoa elimu na ujumbe ulio bora zaidi.

Ikithibitika kwa namna moja au nyingine umehusika kudurufu nakala au kusambaza katika mitandao ya kijamii na mingieyo nakala ya kitabu hiki utakuwa umetenda uharifu chini ya sheria ya makosa ya mtandao. Adhabu ya kifungu au faini au vyote kwa pamoja vinaweza kutolewa dhidi yako. Epuka wizi, kuwa mzalendo kwa kununua kazi za wasanii wetu. Wizi haukubaliki kiimani na hata kijamii.

Hata hivyo, taarifa, ujumbe au mafunzo yanayopatikana katika kitabu hiki hayana uhusiano wowote na matokeo ya msomaji. Mwandishi, mchapishaji au msambazaji hatawajibika kwa tatizo lolote litakalojitokeza kutokana na usomaji wa kitabu hiki.

Shipping and delivery

We are proud to offer international shipping services that currently operate in over 200 countries and islands world wide. Nothing means more to us than bringing our customers great value and service. We will continue to grow to meet the needs of all our customers, delivering a service beyond all expectation anywhere in the world.

How do you ship packages?

Packages from our warehouse in China will be shipped by ePacket or EMS depending on the weight and size of the product. Packages shipped from our US warehouse are shipped through USPS.

Do you ship worldwide?

Yes. We provide free shipping to over 200 countries around the world. However, there are some locations we are unable to ship to. If you happen to be located in one of those countries we will contact you.

What about customs?

We are not responsible for any custom fees once the items have shipped. By purchasing our products, you consent that one or more packages may be shipped to you and may get custom fees when they arrive to your country.

How long does shipping take?

Shipping time varies by location. These are our estimates:

Location *Estimated Shipping Time
United States 10-30 Business days
Canada, Europe 10-30 Business days
Australia, New Zealand 10-30 Business days
Central & South America 15-30 Business days
Asia 10-20 Business days
Africa 15-45 Business days
*This doesn’t include our 2-5 day processing time.

Do you provide tracking information?

Yes, you will receive an email once your order ships that contains your tracking information. If you haven’t received tracking info within 5 days, please contact us.

My tracking says "no information available at the moment".

For some shipping companies, it takes 2-5 business days for the tracking information to update on the system. If your order was placed more than 5 business days ago and there is still no information on your tracking number, please contact us.

Will my items be sent in one package?

For logistical reasons, items in the same purchase will sometimes be sent in separate packages, even if you have specified combined shipping.

If you have any other questions, please contact us and we will do our best to help you out.

Refunds & returns policy

Order cancellation

All orders can be cancelled until they are shipped. If your order has been paid and you need to make a change or cancel an order, you must contact us within 12 hours. Once the packaging and shipping process has started, it can no longer be cancelled.

Refunds

Your satisfaction is our #1 priority. Therefore, you can request a refund or reshipment for ordered products if:

  • You do not receive them within the guaranteed time (45 days not including 2-5 day processing)
  • You receive the wrong item
  • You do not want the product you have received (but you must return the item at your expense and the item must be unused)

We do not issue the refund if:

  • Your order does not arrive due to factors within your control (e.g. providing the wrong shipping address)
  • Your order does not arrive due to exceptional circumstances outside our control (e.g. not cleared by customs, delayed by a natural disaster)
  • Other exceptional circumstances outside the control of store.trisoftnet.co.tz

*You can submit refund requests within 15 days after the guaranteed period for delivery (45 days) has expired. You can do it by sending a message on page.

If you are approved for a refund, then your refund will be processed, and a credit will automatically be applied to your credit card or original method of payment, within 14 days.

Exchanges

If for any reason you would like to exchange your product, perhaps for a different size in clothing. You must contact us first and we will guide you through the steps.

Please do not send your purchase back to us unless we authorise you to do so.

Real customer reviews

2 reviews
100% of buyers enjoyed this product!
5 stars
( 2 )
4 stars
( 0 )
3 stars
( 0 )
2 stars
( 0 )
1 star
( 0 )
  1. Enock

    Superb

  2. Juliana

    Mungu akubariki

Only logged in customers who have purchased this product may leave a review.